VIFO VYA WANAWAKE WAJAWAZITO NA WATOTO VYAPUNGUA MONDULI.

By | 03:06
                                     
Tatizo la vifo vya wanawake  wajawazito na watoto limeanza kupungua wilayani Monduli mkoani Arusha ikiwa ni matokeo ya  wananchi kujitolea kuchangia ujenzi wa zahanati na vituo vya  afya na pia kuhamasika kupokea ushauri wa wataalam wa afya  ukiwemo wa kujiunga na mfuko wa afya ya jamii (CHF).
 Akizungumza wakati wa uzinduzi wa moja ya zahanati zilizojengwa  na wanachi katika kijiji cha NAFCO kaya ya loksale mganga mkuu wa wilaya ya monduli Dr.Zaveri Peter Benela amesema pamoja na changamoto zilizopo ikiwemo ya mila potofu  asilimia  kubwa  ya  wannachi wanaendelea  kubadilika.
 
Mtendaji wa kata ya lokisale Bw.Ahmed Mhando amesema kukamilika  kwa  zahanati ya kijiji cha NAFCO iliyoghaimu zaidi ya milioni 39 pamoja na kuwapunguzia wananchi umbali wa kuzifikia huduma za  afya umewaongezea hamasa ya kujiunga na huduma ya mfuko wa afya yajamiI.
 
Akizungumzia hatua hiyo baada ya kuzindua na kutembelea zahanati hiyo waziri mkuu aliyejiuzulu Mh.Edwad Lowasa amewataka watendaji kuongeza uhamasishaji wa wananchi kujiunga na huduma ya mfuko wa  afya ya jamii.
 
Mh Lowasa ambaye pia ni mbunge  wa Monduli amesema mfuko wa afya  ya jamii ndio njia pekee ya kuwawezesha wananchi kupata tiba wakati wote na kwa gharama nafuu na kwamba licha ya kuwepo kwa  changamoto zinaendele kufanyiwa  kazi.
Newer Post Older Post Home