LIVERPOOL YAMSAJILI DANNY INNGS.

By | 04:21




140810-004-Liverpool_Dortmund

Klabu ya Liverpool imetangaza
kufikia makubaliano na klabu ya Burnley juu
ya usajili wa mshambuliaji wa England Danny Inngs .
Liverpool ambayo msimu huu uliopita imejikuta
ikishindwa kufikia malengo yake baada ya kumaliza
 nje ya nafasi za kufuzu michuano ya ligi ya mabingwa
 imekuwa ikihaha kuhakikisha inasajili wachezaji ambao
 wanaweza kuendana na malengo na ukubwa wa klabu
 hiyo na Danny Inngs amekuwa kwenye orodha
ya kocha Brendan Rogers kwa muda mrefu .
Danny Ings amefunga mabao 11 kwenye msimu uliopita wa EPL.
Danny Ings amefunga mabao 11
 kwenye msimu uliopita wa EPL.
Kinyume na hali ilivyokuwa kwa
klabu yake ya Burnley ambayo imeshuka
daraja Danny Inngs alikuwa na msimu mzuri
 kwake binafsi akiwa ametokea kuwa moja
kati ya washambuliaji tishio kwenye ligi kuu
ya England baada ya kufunga mabao 11 .
Inngs pia alikuwa anatafutwa na klabu kadhaa
nchini England na barani ulaya ambapo kwa
nyakati tofauti Manchester United na Real
 Sociedad ya Hispania zimekuwa zikihaha kusaka saini yake .
Danny Ings ni mshambuliaji wa kimataifa wa England.
Danny Ings ni mshambuliaji wa kimataifa wa England.
Ujio wa Ings huenda ukawa unamaanisha mwisho wa
washambuliaji Mario Balotelli na Rickie Lambert
ambao walishindwa kuonyesha ubora baada ya kusajiliwa msimu uliopita .
Newer Post Older Post Home