MWENYEKITI WA IPP DR REGINALD MENGI ATUNUKIWA TUZO YA MHAMASISHAJI BORA MAENDELEO KWA VIJANA.

By | 04:52

Mwenyekiti wa IPP DR Reginald Mengi ametunukiwa tuzo ya mjasiriamali mhamasishaji bora wa maendeleo kwa vijana.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi ametunukiwa Tuzo ya Mjasiriamali Mhamasishaji na Mchocheaji Bora wa Maendeleo kwa Vijana wa mwaka 2015.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi ametunukiwa Tuzo hiyo jijini Dar es salaam na Chama cha Masoko cha Chuo Kikuu Dar es salaam -DUMA, chenye uhusiano na Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu hicho, wakati wa Tamasha la Masoko la mwaka huu, baada ya kuwashinda wafanyabiashara Mohammed Dewji na Patrick Ngowi walioshindanishwa katika kipengere hicho.
Rais wa DUMA Docta Ulimwengu amesema ushindi wa Dr Mengi na washindi wengine wa tuzo hizo wamepatikana kwa kupigiwa kura na wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya juu nchini.
Akipokea Tuzo hiyo Dr Mengi amewakumbusha vijana kuwa wamezungukwa na fursa nyingi ambazo zinawahitaji wawe na macho yanayoweza kuona fursa hizo ili waweze kuzitumia kujikwamua kiuchumi.
Wakati wa tamasha hilo, DUMA pia imewatunukia tuzo watu wengine wanne ambapo mhe. Zitto Zuberi Kabwe alitunukiwa tuzo ya Mwanasiasa Mhamasishaji Bora wa Vijana baada ya kuwashinda Mhe. Halima Mdee na Mhe. January Makamba, na tuzo hiyo ilipokelewa kwa naiba yake na Prof. Kitilya Mkumbo.
Aidha Bw. Sheria Ngowi alishinda Tuzo yaMwanamitindo Mhamasishaji Bora kwa Vijana baada ya kuwashinda Jokate Mwigelo na Martin Kadinda.
Pia Mtangazaji Kijana Millard Ayo ametunukiwa Tuzo yaMwanahabari Mhamasishaji Bora wa vijana ya kumshinda mtangazaji mwenzake Salama Jabir.
Naye Mwanamuziki Diamond Platnum ametunukiwa tuzo ya Mwanamuziki Mhamasishaji bora wa Vijana baada ya kuwashinda wanamuziki wenzake Vanessa Mdee na Ali Kiba.
Tuzo za washindi hao zilipokelewa kwa niaba yao wawakilishi wao baada ya wahusika kuwa nje ya jiji la Dar es salaam kwa sababu maalum.

Newer Post Older Post Home