RAFAEL BENITEZ AANZA KUTUNISHIANA MISULI NA UONGOZI WA REAL MADRID.

By | 06:24




1433149-30659858-1600-900

Zikiwa zimepita siku tano pekee tangu
Rafael Benitez alipotambulishwa kuwa
kocha mpya wa Real Madrid kufuatia
klabu hiyo kumfukuza kazi Mtaliano
 Carlo Ancelotti , tayari kocha huyu mpya ameanza
kutunishiana misuli na uongozi wa klabu hii ya kifalme
yenye maskani yake katikati ya mji mkuu wa Hispania .
Rafael Benitez kwa mujibu wa ripoti zilizoibuka hii leo
ametofautiana maoni na bosi wake ambaye ni rais wa
 klabu hiyo Florentino Perez juu ya mshambuliaji
atayaesajiliwa na klabu hiyo ili kuimairisha kikosi
chake cha msimu wa mwaka 2015/2016.
Gazeti moja la kila siku nchini Hispania la habari za
michezo limeripoti kuwa Rafael Benitez anataka
 kumrudisha mshambuliaji aliyeuzwa toka
 Madrid Alvaro Morata baada ya kuridhishwa
na kiwango alichokionyesha msimu huu .
Rafa Benitez amependekeza kusajiliwa kwa mshambuliaji wa Juventus Alvaro Moratta.
Rafa Benitez amependekeza kusajiliwa kwa
 mshambuliaji wa Juventus Alvaro Moratta.
Matamanio haya ya Benitez kumsajili Alvaro
Moratta yanakwenda kinyume na Perez
ambaye anataka kumsajili Sergio Aguerro
 ili aweze kuiongoza safu ya mashambulizi ya
 Real Madrid kwa ajili ya msimu ujao .
Perez amekuwa na utamaduni wa kusajili wachezaji
nyota wenye majina makubwa kwa karibu kila msimu
ili kuifanya klabu hiyo itengeneze fedha kutokana na
biashara inayofanyika nje ya uwanja .
Florentino Perez na kocha mpya Rafa Benitez wameripotiwa kutofautiana juu ya mshambuliaji wa kumsajili.
Florentino Perez na kocha mpya Rafa Benitez wameripotiwa kutofautiana
 juu ya mshambuliaji wa kumsajili.
Hata hivyo bado haijafahamika kama tofauti hii inaweza kuwa na athari
yoyote kwenye ufanyaji kazi wa Rafa Benitez lakini itakuwa ishara ya
 kwanza ya aina ya mazingira ambayo anatajia kuyakuta akiwa
ameanza kazi rasmi kama kocha wa moja kati ya klabu kubwa kuliko zote duniani .
Newer Post Older Post Home