HABARI

MICHEZO

The Latest

Nguesso

Image copyright
Image captionSassou Nguesso ameongoza Congo-Brazzaville kwa miaka 30

Wapiga kura katika Jamhuri ya Congo wameidhinisha marekebisho ya katiba yanayomruhusu rais wa sasa kuwania kwa muhula wa tatu.
Kwa mujibu wa matokeo rasmi, asilimia 92 ya wapiga kura walioshiriki kura ya maamuzi kuhusu marekebisho hayo ya kikatiba Jumapili waliunga mkono marekebisho hayo.
Kuandaliwa kwa kura hiyo ya maamuzi kulikuwa kumezua maandamano wiki iliyopita na vyama vikuu vya upinzani viliisusia.
Muungano wa Ulaya na Marekani zimekashifu kuandaliwa kwa kura hiyo, na kusema mazingra nchini Congo hayakuwa mwafaka kuwezesha kuandaliwa kwa kura ya maamuzi huru na ya haki.
Mwandishi wa BBC katika taifa jirani la DR Congo Maud Jullien anasema takwimu kutoka kwa tume ya taifa ya uchaguzi zinaonyesha zaidi ya asilimia 70 ya wapiga kura walishiriki.
Lakini kiongozi wa upinzani ameambia BBC kwamba hawatambui matokeo hayo na kudai kwamba kulikuwa na udanganyifu. Amesema watu wengi hawakujitokeza kupiga kura.
Chini ya katiba ambayo imekuwepo, Rais Denis Sassou Nguesso alikuwa haruhusiwi kuwania kwa muhula mwingine kwa sababu amepitisha umri wa miaka 71 na pia amehudumu mihula miwili tayari.

Nguesso
Image captionKulikuwa na wengine walioandamana kumuunga mkono

Rais Sassou Nguesso aliingia mamlakani mara ya kwanza mwaka 1979.
Kwa sasa anamalizika muhula wa pili wa miaka saba. Alishinda uchaguzi mkuu wa majuzi zaidi 2009 kwa karibu asilimia 79. Uchaguzi huo ulisusiwa na nusu ya wagombea wa upinzani.
Rais Sassou Nguesso ni miongoni mwa viongozi wa sasa Afrika waliokaa madarakani muda mrefu zaidi.

Tume ya Uchaguzi Zanzibar imetoa matokeo ya uchaguzi wa rais ambayo yamehakikiwa kutoka baadhi ya maeneo visiwani humo. Kufikia sasa tume hiyo imetangaza matokeo kutoa majimbo 13 kati ya 54.

Matokeo hayo yaliyokuwa yametangazwa kufikia saa tatu asubuhi Oktoba 27 ni kama ifuatavyo:
Zanzibar ina jumla ya wapiga kura 503,860 waliojiandikisha kupiga kura, kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar.


Image copyrightAP
Image captionToyota ndio gari maarufu zaidi duniani mwaka huu
Sasa ni rasmi Toyota ndiyo gari maarufu zaidi duniani.
Kampuni hiyo ya kutengeneza magari ya Japan imeipiku Volkswagen kutoka kwenye nafasi ya kwanza ya orodha ya makampuni yaliyouza idadi kubwa zaidi ya magari duniani mwaka huu.
Yamkini Toyota imeuza takriban magari milioni 7.5 katika kipindi cha miezi tisa ya mwaka huu.
Wapinzani wao wa karibu Volkswagen kwa upande wao wameuza magari milioni 7.43.
Nafasi ya tatu inashikiliwa na kampuni ya kutengeneza magari ya Marekani, General Motors.
Image captionToyota imeuza takriban magari milioni 7.5 katika kipindi cha miezi tisa ya mwaka huu
GM iliuza magari milioni 7.2 katika kipindi hicho cha miezi 9 ya mwanzo wa mwaka huu.
Wadadisi wanasema kuwa sakata ya udanganyifu iliyoikumba kampuni hiyo ya ujerumani itaathiri zaidi mauzo yake katika siku za hivi punde.
Volkswagen ilipatikana na hatia ya kupandikiza programu ya siri katika injini ya magari yake yanayotumia mafuta ya dizel ilikudanganya wachunguzi wa utendakazi wake kuhusina na kiwango cha hewa chafu inayotoa.
Licha ya kushikilia nafasi ya kwanza Toyota bado haijatimiza malengo yake ya kuuza idadi ya magari sawa na ilivyouzwa katika kipindi sawa na hicho mwaka uliopita.
Image copyrightToyota
Image captionKampuni hiyo ya Japan iliipiku GM kwa mara ya kwanza mwaka wa 2008.
Kampuni hiyo ya Japan iliipiku GM kwa mara ya kwanza mwaka wa 2008.
Tangu hapo Toyota imekuwa ikiendelea kunawiri isipokuwa mwaka wa 2011 iliposhindwa kusafirisha magari baada ya dukuduku na hofu kuenea kuwa huenda miale ya sumu ya nyuklia ilikuwa imeenea kwenye magari yao.
Mwaka huo kimbunga kikubwa kiliikumba kisiwa chenye karakana za Toyota Kaskazini Mashariki mwa Japan na kuathiri utendakazi wake.

Mourinho


Image copyrightEPA
Image captionKlabu ya Chelsea imekuwa ikiandikisha matokeo mabaya msimu huu

Jose Mourinho amefunguliwa mashtaka ya utovu wa nidhamu na Shirikisho la Soka la Uingereza kwa sababu ya lugha aliyoitumia na vitendo vyake wakati wa mechi ambayo Chelsea walichapwa na West Ham United wikendi.
Mourinho alifukuzwa eneo la marefa uwanjani baada yake kwenda kutaka kuzungumza na refa Jon Moss katika chumba chake wakati wa mapumziko mechi hiyo ya Jumamosi.
Klabu zote mbili pia zimeshtakiwa kwa kushindwa kudhibiti wachezaji na zimepewa hadi Oktoba 29 kujibu mashtaka hayo.
Chelsea tayari wanakabiliwa na faini ya £25,000 kwa wachezaji zaidi ya watano kupewa kadi za manjano wakati wa mechi hiyo ya Ligi ya Premia.
Kando na kadi mbili alizoonyeshwa Nemanja Matic, Chelsea pia walishuhudia wachezaji wao Cesar Azpilicueta, Willian, Cesc Fabregas, John Mikel Obi na Diego Costa wakilishwa kadi uwanjani Upton Park.

MaticImage copyrightReuters
Image captionMatic alipewa kadi mbili za manjano

Msaidizi wa Mourinho Silvino Louro pia alifukuzwa eneo lake wakati wa mechi hiyo na vilevile ameshtakiwa kwa utovu wa nidhamu.
Klabu hiyo pia itatakiwa kueleza wasimamizi wa Ligi ya Premia ni kwa nini Mourinho alikosa kuzungumza na wanahabari baada ya mechi hiyo.
Mechi hiyo ilikuwa ya tano kwa Chelsea kushindwa katika mechi 10 za ligi msimu huu na inawaacha mabingwa hao watetezi wakiwa nambari 15 na alama 11, alama 11 nyuma ya viongozi Manchester City.

Nigel Owens

Image copyrightGetty
Image captionNigel Owens anatoka Wales


Owens alisema kupitia mitandao ya kijamii kwamba anashukuru sana kutunukiwa hadhi hiyo.
New Zealand walicharaza Afrika Kusini 20-18 Jumamosi na watakutana na Australia, waliowashinda Argentina 29-15 Jumapili.
Mataifa hayo mawili hayajawahi kukutana kwenye fainali.
Mwingereza Ed Morrison, aliyekuwa refa fainali ya 1995 kati ya Afrika Kusini na New Zealand, na raia wa Ireland Alain Rolland, aliyesimamia fainali kati ya England na Afrika Kusini 2007, ndio marefa wengine kutoka kaskazini waliowahi kusimamia fainali ya dimba hilo.
Mwakilishi wa New Zealand jopo la kuteua refa wa kusimamia fainali Bw Grant Fox alikuwa tayari amedokeza kwamba Owens angesimamia mechi hiyo ya Oktoba 31 uwanjani Twickenham.

Image captionKatibu mkuu wa shirikisho la soka ulaya,uefa, Gianni Infantino
Katibu mkuu wa shirikisho la soka barani ulaya (Uefa) muitaliano Gianni Infantino amejitosa kwenye kinyang"anyiro cha kuwania kiti cha uraisi wa shirikisho la soka dunia Fifa.
Infantino, anaunga na boss wa Uefa aliyesimamishwa Mfaransa Michel Platini, kuwania nafasi hiyo kuongoza chombo hicho cha soka.
Huku rais wa shirikisho la soka la Asia Sheikh Salman bin Ebrahim Al Khalifa pia amethibitisha kuwania cheo hicho.
Wengine wanaowania kiti hicho cha urais wa Fifa ni Mosima Gabriel maarufu kama Tokyo Sexwale, wa Afrika Kusini Prince Ali Bin al-Hussein wa Jordan, David Nakhid, wa Trinidad and Tobago, Jerome Champagne Musa Bility na Segun Odegbami wa Nigeria


Mawaziri watano wa Serikali inayomaliza muda wake wameanguka kwenye uchaguzi majimboni mwao, sambamba na wagombea wengine maarufu wa Bunge lililopita baada ya matokeo ya kura zilizopigwa Jumapili kuanza kutangazwa jana.

Mawaziri hao wanaungana na wabunge wengine maarufu wa Bunge la Kumi walioshindwa kutetea majimbo yao, wakiwamo wa kambi ya upinzani ambao wameangushwa na wagombea wa CCM.
Pia wamo mawaziri wa zamani wawili, Cyril Chami na Omary Nundu walioanguka kwenye uchaguzi, kwa mujibu wa matokeo ambayo yanaendelea kutangazwa.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema jana kuwa itakamilisha kazi ya kutangaza matokeo yote keshokutwa.

Mawaziri walioanguka kwenye uchaguzi huo ni Steven Wasira, Christopher Chiza, Aggrey Mwanri, Dk Steven Kebwe na Anne Kilango.

Katika matokeo yaliyotangazwa jana, Wasira, kada maarufu na mwanasiasa mkongwe aliyekuwa akitetea Jimbo la Bunda, alijikuta akiangushwa na mwanasiasa kijana, Ester Bulaya, ambaye alihamia Chadema baada ya Bunge la Kumi kumaliza muda wake.

Wasira, ambaye alikuwa Waziri wa Kilimo na Chakula, alianza mchakato wa uchaguzi mwaka huu kwa kuomba ridhaa ya CCM agombea urais, lakini hakupitishwa. Bulaya, ambaye alikuwa mbunge wa viti maalum (CCM), alipata kura 28, 508 na kumuacha mbali waziri huyo mkongwe aliyepata kura 19, 126.

Mwingine aliyeanguka ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu- Uwezeshaji na Uwekezaji, Christopher Chiza ambaye ameangushwa na Bilago Samson wa Chadema katika Jimbo la Buyungu. Waziri huyo alizidiwa kwa kura 104 baada ya Samson kupata kura 23,041 dhidi ya 22,934 za Chiza.

Lakini hali haikuwa hivyo kwa Naibu Waziri wa Tamisemi, Aggrey Mwanri kwenye Jimbo la Siha. Waziri huyo alizidiwa kwa zaidi ya kura 4,100 na mpinzani wake kutoka Chadema, Dk Godwin Mollel aliyepata kura 22,746.

Katika Jimbo la Serengeti, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Stephen Kebwe pia alijikuta akipoteza nafasi ya kurudi bungeni kwa kura alipoangushwa na Marwa Ryoba wa Chadema. Dk Kebwe alipata kura 39,232, akiwa amezidiwa na mpinzani wake kwa zaidi ya kura 820.

Anne Kilango, ambaye aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Elimu mwaka 2013 baada ya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyosababishwa na kashfa ya Operesheni Tokomeza, ameangushwa na mgombea wa Chadema, Naghenjwa Kaboyoko wa Chadema kwa tofauti ya kura 3,297.

Kilango alipata kura 15,539 wakati mgombea huyo wa Chadema alipata kura 18,836. Pia wabunge maarufu kama Vincent Nyerere (Musoma Mjini), James Lembeli (Kahama Mjini) na Kyisieri Chambiri (Babati Mjini) wameangushwa.

Nyerere, aliyekuwa akitetea kiti cha Musoma Mjini kwa tiketi ya Chadema, aliachwa mbali na mgombea wa CCM, Vedastus Mathayo aliyepata kura 32, 836 dhidi ya 25,549.43 za Nyerere.
Lembeli, ambaye alihamia Chadema muda mfupi baada ya Bunge la Kumi kumaliza muda wake, aliachwa mbali na mfanyabiashara maarufu, Jumanne Kishimba aliyepata kura 47,553 dhidi ya kura 30,122 za Lembeli.

Walioshinda
Wakati hao wakidondoka wabunge wengine wameendelea kutetea majimbo yao kwa kupata kura za kishindo, wakiongozwa na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliyetetea jimbo lake la Hai, Joshua Nassar (Chadema, Arumeru Mashariki), Stephen Masele (CCM, Shinyanga Mjini), Jenister Mhagama (CCM, Peramiho), Silvestry Koka (CCM, Kibaha), David Silinde (Chadema,Momba), Aesh Hilaly (CCM, Sumbawanga Mjini), Joseph Selasini (Chadema,Rombo), Profesa Jumanne Maghembe (CCM Mwanga).

Jimbo la Tunduma
Ubunge: Mwakajoka Frank (Chadema) 32,442, Frank Sichalwe (CCM) 17,220, James Mwakalonge (TLP) 85, Reddy Makuba (ACT Wazalendo) , 319.

Jimbo la Tarime Mjini
Ubunge: Ester Matiko (Chadema) 20,017, Michael Kembaki (CCM), 14, 025, Deogratias Meck (ACT-Wazalendo) 356.

Jimbo la Siha
Ubunge: Dk Godwin Mollel (Chadema) 22,746 na Aggrey Mwanry (CCM) 18,584.


Jimbo la Buyungu
Ubunge: Kasuku Bilago (Chadema), 23,041, Christopher Chiza (CCM) 22,934, Athanas Mawazo (NCCR-Mageuzi) 1,237 na Leopold Muahanga(ACT Wazalendo).

Jimbo la Lindi Mjini
Ubunge: Selemani Kaunje (CCM) 20,733 na Salum Barwany (CUF) 18, 843.

Jimbo la Mkinga
Ubunge: Dustan Kitandula (CCM) 21,623, Bakari Kassimu (CUF) 13, 547, Rachel Sadick (Chadema) 3,789 na Ali Mwita (ACT Wazalendo) 402.

Jimbo la Tandahimba
Ubunge: Ahmad Katani (CUF) 55,156, Shaibu Likumbo (CCM) 41,088 na Hamis Hassan (ADC) 966.

Jimbo la Mbinga Mjini
Ubunge: Sixtus Mapunda (CCM) 28,364 na Mario Milinga(Chadema) 102.

Jimbo la Mbinga Vijijini
Ubunge: Martin Msuha (CCM) 59, 269 na Benjamin Akitanda (Chadema) 11, 285.

Jimbo la Nzega Mjini
Ubunge: Hussein Bashe (CCM) 18,754, Charles Mabula(Chadema) 9,658, Kitwana Abdallah (ACT Wazalendo) 180 na Leonard John(CUF) 95.

Jimbo la Peramiho
Ubunge: Jenista Mhagama (CCM) 32,057, Mwingira Erasmo (Chadema) 11,462 na Claudius Claudius(DP) 217.

Jimbo la Musoma Mjini
Ubunge: Vedastus Mathayo (CCM) 32, 836, Vincent Nyerere (Chadema) 25, 549, Esseko Tongola (ACT Wazalendo) 513, Gabriel Ocharo (CUF) 186, Maimuna Matola (ADC) 50, Ibrahim Selemani (Tadea) 21, Rutaga Sospeter (AFP) 25 na Makongoro Jumanne (UMD) 19.

Jimbo la Geita Mjini
Ubunge: Kanyasu John (CCM) 34, 953, Rogers Ruhega (Chadema) 26, 303 na Malebo Michael (CUF) 625.

Jimbo la Monduli
Ubunge: Julius Kalanga (Chadema) 35,025, Namelock Sokoine (CCM) 25,925 na Navaya Ndaskoi (ACT Wazalendo) 367.

Jimbo la Kibaha Mjini
Ubunge: Silvestry Koka (CCM) 31,462, Paul Mtally (Chadema) 24,860, Habibu Mchange (ACT Wazalendo) 3,438, Gombati Waziri (CCK) 259, Betha Mpata (APPT), 120 na Kibona Ally (AFP) 108.

Jimbo la Arumeru Mashariki
Ubunge: Joshua Nassari (Chadema) 86, 694, Pallaghyo John (CCM) 31, 847, Batuli Ismail (ACT Wazalendo) na Mgina Ibrahim (AFP) 236.

Jimbo la Serengeti
Ubunge: Marwa Ryoba (Chadema) 40, 059, Dk Stephen Kebwe (CCM) 39, 232, Burito Thomas (ACT Wazalendo) 1, 445, Imakulata Mniko (CUF) 328 na Mosena Nyambabe (NCCR-Mageuzi) 408.

Jimbo la Kahama Mjini
Ubunge: Jumanne Kishimba (CCM) 47,553, James Lembeli (Chadema) 30,122 na Bobson Wambura (ACT Wazalendo) 605.

Jimbo la Babati Mjini
Ubunge: Pauline Gekul (Chadema) 21,970 na Kisyeri Chambiri (CCM) 16,434.

Jimbo la Shinyanga Mjini
Ubunge: Steven Masele (CCM) 35,858, Patrobas Katambi (Chadema) 31,027, Nyangaki Shilungushela (ACT Wazalendo) 411 na Emiliana Tambwe (APPT) 178.

Jimbo la Moshi Mjini
Ubunge: Jaffar Michael (Chadema) 51,646, Davis Mosha(CCM) 26,920, Buni Ramole (ACT-Wazalendo) 634, Issack Kireti (Sau) 181 na Godlisen Kitali (UDP) 35.

Jimbo la Dodoma Mjini
Ubunge: Antony Mavunde (CCM) 84,512, Benson Kigaila (Chadema), 42, 140 na Christina Alex (ACT Wazalendo) 927.

Jimbo la Njombe Kaskazini
Ubunge: Joram Hongoli (CCM) 20, 430 na Edwin Swale (Chadema) 10, 407.


Jimbo la Kondoa Mjini
Ubunge: Edwin Sanda (CCM) 13, 333, Ally Kambi (CUF) 6,783, Misanya Ally (Chadema) 1,822, Maulid Majala (ACT Wazalendo) na Salimu Rashidi (UDP) 53.

Jimbo la Bukombe
Ubunge: Dotto Biteko (CCM) 47,147, Profesa Kulikoyela Kahigi (Chadema) 29,929 na Dick Bagamba (ACT Wazalendo) 1,673.

Jimbo la Bunda Mjini
Ubunge: Ester Bulaya (Chadema) 28, 508, Stephen Wasira (CCM) 19, 126 na Maganya Kulwa (ACT Wazalendo) 293.

Jimbo la Tarime Vijijini
Ubunge: John Heche (Chadema) 47,249, Christopher Kangoye (CCM) 42,325, Charles Mwera (ACT Wazalendo) 1,846 na Tingwa Migera (Chausta) 367.

Jimbo la Hai
Ubunge: Freeman Mbowe (Chadema) 51,124, Danstan Mallya (CCM) 26,996, Nuru Mohammed (ACT-Wazalendo) 318 na Ndashuka Issack (APPT-Maendeleo) 279.

Jimbo la Mbogwe
Ubunge: Augustino Masele (CCM) 32,921, Nicodemus Maganga (Chadema) 13,975 na Andrew Mnuke (ACT Wazalendo) 5,464.
Jimbo la Busega
Ubunge: Dk Raphael Chegeni (CCM) 40,977, David William (Chadema) 26,995 na Zangi Robart (UDP) 802.
Jimbo la Msalala
Ubunge: Ezekiel Maige (CCM) 36,010, Paulo Malaika(Chadema) 20, 124, Marco Suwa (ACT Wazalendo) 672 na Abeid Ibeshi (UDP) 251.
Jimbo la Ngara
Ubunge: Alex Gashaza (CCM) 53,387, Dk Bujari Simon (Chadema) 35,254, Helen Gozi (NCCR-Mageuzi) 997 na Dotto Jasson Bahemu (ACT Wazalendo) 440.
Jimbo la Kisarawe
Ubunge: Seleman Jaffo (CCM) 28, 054, Rashid Mwishehe (CUF) 8, 863 na Asha Chuma (UDP) 364.
Jimbo la Bagamoyo
Ubunge: Dk Shukuru Kawambwa (CCM) 26,434, Andrew Kasambala (CUF) 16,330, Mwamini Saidi (UMD) 418 na Saidi Athman (ACT Wazalendo) 418.
Jimbo la Ilemela
Ubunge: Angelina Mabula (CCM) 85,424, Highness Kiwia(Chadema) 61, 679 na Addam Kimwaga (ACT Wazalendo) 3,910.
Jimbo la Bukoba Mjini
Ubunge: Wilfred Lwakatare (Chadema) alipata kura 28, 112 na kumshinda Balozi Khamis Kagasheki (CCM) aliyepata kura 25, 565.
Jimbo la Ilala
Ubunge: Mussa Azzan Zungu wa CCM alishinda kwa kupata kura 35,518 dhidi ya Hassanal Rajabal wa Chadema aliyepata kura 32,333.


Image captionMbwa ampiga risasi mmiliki wake !

Na katika kisa ambacho kimewaacha watu wengi kote duniani wamepigwa na butwaa,,,,
Mwanamke mmoja mmiliki wa mbwa huko Marekani alilazwa hospitalini baada ya jibwa lake kufyatua bastola na kumjeruhi mguu.
Amini usiamini ni tukio la kweli kabisa.
Afisa wa mazingira wa jimbo la, Indiana, Jonathon Boyd amenukuliwa akisema kuwa bi Allie Carter alikuwa ameenda kuwinda bata wa mwituni akiwa amejihami na bastola yake na jibwa lake.
''Baada ya muda akawa anahisi amechoka kisha akaweka bastola yake chini.''
''Kwa bahati mbaya jibwa hilo lilikanyaga bunduki hiyo na kufyatua risasi iliyomjeruhi bi Carter mguuni.''

Image captionKwa bahati mbaya jibwa hilo lilikanyaga bunduki hiyo na kufyatua risasi

Boyd anasema kuwa bibi huyo alijeruhiwa vidole vya mguuni lakini amepata matibabu.
Afisa huyo aliongezea kusema kuwa bi Carter hajakamilisha mafunzo ya msingi kabla hajaruhusiwa kuwa mwindaji na hivyo akasema huenda ajali hiyo ingeepukwa ikiwa angekuwa amekamilisha mafunzo hayo.
Ukistaajabu ya Musa ,,,,,,,

Chanzo: Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania

24. Jimbo la Kiwani, Kusini Pemba
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT270.44
Chifu YembaADC711.15
John MagufuliCCM1,66126.91
Edward LowassaCHADEMA4,22968.51
Hashim SpundaCHAUMA961.56
Janken KasambalaNRA280.45
Macmillan LyimoTLP220.36
Fahmi DovutwaUPDP390.63
23. Jimbo la Donge, Kaskazini Unguja
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT50.07
Chifu YembaADC220.33
John MagufuliCCM5,59283.69
Edward LowassaCHADEMA1,01915.25
Hashim SPundaCHAUMA230.34
Janken KasambalaNRA100.15
Macmillan LyimoTLP40.06
Fahmi DovutwaUPDP70.10
22. Jimbo la Mkoani, Kusini Pemba
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT200.18
Chifu YembaADC600.55
John MagufuliCCM3,34130.43
Edward LowassaCHADEMA7,36867.10
Hashim SpundaCHAUMA870.79
Janken KasambalaNRA440.40
Macmillan LyimoTLP330.30
Fahmi DovutwaUPDP270.25
21. Jimbo la Ndanda, Mtwara
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT5941.10
Chifu yembaADC4090.76
John MagufuliCCM33,69962.34
Edward LowassaCHADEMA19,01735.18
Hashim SpundaCHAUMA1890.35
Janken KasambalaNRA470.09
Macmillan LyimoTLP510.09
Fahmi DovutwaUPDP490.09
20. Jimbo la Kiwengwa, Kaskazini Unguja
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT150.33
Chifu YembaADC240.53
John MagufuliCCM3,31773.30
Edward LowassaCHADEMA1,10424.40
Hashim SpundaCHAUMA270.60
Janken KasambalaNRA90.20
Macmillan LyimoTLP190.42
Fahmi DovutwaUPDP100.22
19. Jimbo la Mtambile, Kusini Pemba
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT70.10
Chifu YembaADC410.59
John MagufuliCCM90212.99
Edward LowassaCHADEMA5,87584.58
Hashim SpundaCHAUMA560.81
Janken KasambalaNRA220.32
Macmillan LyimoTLP180.26
Fahmi DovutwaUPDP250.36
18. Jimbo na Nsimbo, Katavi
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT1830.48
Chifu yembaADC640.17
John MagufuliCCM31,41383.14
Edward LowassaCHADEMA6,04215.99
Hashim SpundaCHAUMA460.12
Janken KasambalaNRA60.02
Macmillan LyimoTLP140.04
Fahmi DovutwaUPDP150.04
17. Jimbo la Wete, Kaskazini Pemba
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT180.29
Chifu YembaADC220.36
John MagufuliCCM95815.50
Edward LowasaCHADEMA5,11982.80
Hashim SpundaCHAUMA280.45
Janken KasambalaNRA110.18
Macmillan LyimoTLP160.26
Fahmi DovutwaUPDP100.16
16.Jimbo la Peramiho, Ruvuma
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT3590.81
Chifu YembaADC1350.30
John MagufuliCCM32,50573.20
Edward LowasaCHADEMA11,29125.43
Hashim SpundaCHAUMA660.15
Janken KasambalaNRA160.04
Macmillan LyimoTLP130.03
15.Jimbo la Nanyamba, Mtwara
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MgwiraACT3610.84
Chifu YembaADC2020.47
John MagufuliCCM24,90458.21
Edward LowasaCHADEMA16,99239.72
Hashim SpundaCHAUMA1720.40
Janken KasambalaNRA390.09
Macmillan LyimoTLP480.11
Fahmi DovutwaUPDP640.15
14.Jimbo la Mtambwe , Kaskazini Pemba
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MgwiraACT90.12
Chifu YembaADC280.37
John MagufuliCCM4285.70
Edward LowasaCHADEMA6,93792.33
Hashim SpundaCHAUMA580.77
Janken KasambalaNRA120.16
Macmillan LyimoTLP210.28
Fahmi DovutwaUPDP200.27
13.Jimbo la Moshi Mjini , Kilimanjaro
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MgwiraACT1490.19
Chifu YembaADC1860.23
John MagufuliCCM28,90936.23
Edward LowasaCHADEMA49,37961,88
Hashim SpundaCHAUMA1,1541.45
Janken KasambalaNRA80.01
Macmillan LyimoTLP70.01
Fahmi DovutwaUPDP60.01
12. Jimbo la Mkinga, Tanga
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT2240.56
Chifu YembaADC1860.47
John MagufuliCCM23,79859.81
Edward LowasaCHADEMA15,14238.06
Hashim SpundaCHAUMA3510.88
Janken KasambalaNRA310.08
Macmillan LyimoTLP290.07
Fahmi DovutwaUPDP270.07
11.Jimbo la Mgogoni, Kaskazini Pemba
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT120.16
Chifu YembaADC310.42
John MagufuliCCM7109.59
Edward LowasaCHADEMA6,50687.91
Hashim SpundaCHAUMA891.20
Janken KasambalaNRA120.16
Macmillan LyimoTLP80.11
Fahmi DovutwaUPDP330.45
10.Jimbo la Mbinga Mjini, Ruvuma
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MgwiraACT3290.79
Chifu YembaADC1610.39
John MagufuliCCM29,29570.44
Edward LowasaCHADEMA11,69528.12
Hashin SpundaCHAUMA660.16
Janken KasambalaNRA100.02
Macmillan LyimoTLP160.04
Fahmi DovutwaUPDP160.04
9.Jimbo la Kojani, Kaskazini Pemba
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT270.23
Chifu YembaADC360.30
John MagufuliCCM1,56113.21
Edward LowasaCHADEMA9,98284.50
Hashim SpundaCHAUMA1080.91
Janken KasambalaNRA540.46
Macmillan LyimoTLP270.23
Fahmi DovutwaUPDP180.15
8. Jimbo la Kisarawe, Pwani
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT2350.62
Chifu YembaADC1900.50
John MagufuliCCM24,08663.36
Edward LowasaCHADEMA13,09334.44
Hashim SpundaCHAUMA3140.83
Janken KasambalaNRA260.07
Macmillan LyimoTLP220.06
Fahmi DovutwaUPDP460.12


Image captionJimbo: Gando Mkoa: Kaskazini Pemba

7.Jimbo la Gando, Kaskazini Pemba
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT110.16
Chifu YembaADC230.33
John MagufuliCCM88112.74
Edward LowasaCHADEMA5,90385.34
Hashim SpundaCHAUMA490.71
Janken KasambalaNRA140.20
Macmillan LyimoTLP110.16
Fahmi DovutwaUPDP250.36
6. Jimbo la Chambani, Kusini Pemba
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT150.24
Chifu YembaADC500.79
John MagufuliCCM81812.90
Edward LowassaCHADEMA5,31983.90
Hashim SpundaCHAUMA630.99
Janken KasambalaNRA200.32
Macmillan LyimoTLP190.30
Fahmi DovutwaUPDP360.57
5. Jimbo la Kibaha Mjini, Pwani
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT3140.52
Chifu YembaADC590.10
John MagufuliCCM34,60457.15
Edward LowassaCHADEMA25,44842.03
Hashim SpundaCHAUMA770.13
Janken KasambalaNRA150.02
Macmillan LyimoTLP160.03
Fahmi DovutwaUPDP110.02
4. Jimbo la Bumbuli, Tanga
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT4471.02
Chifu YembaADC1880.43
John MagufuliCCM35,31080.23
Edward LowassaCHADEMA7,92818.01
Hashim SpundaCHAUMA850.19
Janken KasambalaNRA150.03
Macmillan LyimoTLP130.03
Fahmi NasoroUPDP250.06
3. Jimbo la Paje, Kusini Unguja
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT360.45
Chifu yembaADC210.26
John MagufuliCCM6,03575.00
Edward LowassaCHADEMA1,89923.60
Hashim SpundaCHAUMA280.35
Janken KasambalaNRA80.10
Macmilla LyimoTLP80.10
Fahmi DovutwaUPDP70.09
2. Jimbo la Lulindi, Mtwara
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT5281.19
Chifu YembaADC3620.82
John MagufuliCCM31,60871.28
Edward LowassaCHADEMA11,54326.03
Hashim SpundaCHAUMA1790.40
Janken KasambalaNRA430.10
Macmillan LyimoTLP450.10
Fahmi DovutwaUPDP340.08
1. Jimbo la Makunduchi, Kusini Unguja
JinaChamaKuraAsilimia
Anna MghwiraACT220.21
Chifu YembaADC580.56
John MagufuliCCM8,40681.20
Edward LowassaCHADEMA1,76917.09
Hashim SpundaCHAUMA680.66
Janken KasambalaNRA230.22
Macmillan LyimoTLP180.17
Fahmi DovutwaUPDP180.17