Mabehewa 50 Kati ya 274 ya Kusafirishia Mizigo Katika Reli ya Kati Yawasili Nchini Kutoka India.

By | 08:56

.
                    
Mabehewa Hamsini kati ya 274 ya kusafirishia mizigo  katika Reli ya Kati  yamewasili nchini  kutoka India  na mabehewa 22 ya abiria yana tarajiwa kuwasili  Desemba mwaka huu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya U chukuzi  Dakta  SHABANI MWINJAKA amesema kuwasili kwa mabehewa hayo kutaokoa kwa kiasi kikubwa miundombinu ya barabara ambayo huharibika muda mfupi baada ya kutengenezwa kutokana na malori ya mizigo kwani kwa sasa mizigo yote itasafirishwa kwa njia ya reli .
AmesemaKampuni ya Reli T anzania imetengewa zaidi ya shilingi bilioni 45 kwa ajili ya kuboresha huduma zake ikiwa ni pamoja na kununua vichwa na mabehewa mapya.
Amesema  hadi mwaka  2015 injini 45 zitakuwa z imekamilika amba zo z itawezesha kusafirisha tani milioni 1.5 na kuongeza kuwa u jenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es salaam kwenda Kigoma, Tabora hadi Mwanza na Uvinza Msongati hadi B urundi utafanyika.
Mkurugenzi M tendaji wa  Kampuni ya Reli Tanzania M handisi KIPALLO KISAMFU amesema  injini nne zilizokuwa zikitengenezwa mkoani M orogoro zimekamilika na  nyingine 15 zinatengenezwa Afrika ya K usini amba zo z itagharimu  shilingi  bilioni 70 .
Newer Post Older Post Home