
Christiano Ronaldo akisherehekea bao lake dhidi ya Barcelona
Aliyekuwa
msaidizi wa kocha wa Manchester united Mike Phelan anaamini kuwa
Cristiano Ronaldo huenda akaandikisha mkataba wa kurudi katika kilabu ya
Old Trafford katika siku zijazo.
Ronaldo amehusishwa na mpango wa kurudi Manchester United katika muda wake katika kilabu ya Real Madrid ,lakini mpango kama huo haujazaa matunda kufikia sasa.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 ambaye alichezea Man U anafurahia maisha yake katika klabu ya Real Madrid lakini Phelan anaamini huenda akashawishika kurudi katika ligi ya Uingereza.