BASI LA BUNDA EXPRESS LAPINDUKA JIJINI MWANZA.

By | 05:10
                  
Watu wanne wamejeruhiwa katika ajari ya basi iliyotokea katika eneo la Tanesco barabara ya Kenyatta Jijini Mwanza.
Ajali hiyo ilitokea hii leo majira ya saa kumi na moja za alfajiri kwa imehusisha basi la Bunda express lenye namba za usajili T 318 CXZ, lililokuwa likitokea Kituo Cha Mabasi Buzuruga kuelekea Kituo cha Mabasi Nyegezi ambapo.
Chanzo cha ajali hiyo ni baada ya dereva kushindwa kukwepa gari la kushindilia barabara lililokuwa limepaki katika Barabara  Kenyata eneo la eneo la Tanesco ambapo kuna matengenezo ya barabara.

Dakitari wa  zamu wa hospitali ya Rufaa ya Bugando ambapo majeruhi hao wamepelekwa Edwini Mbwambo aliwataja majeruhi hao kuwa ni Alfan Yusufu (50),Christian Iyakugilwa (65), Richard Malema (30),Valentine Kalamagangara (30)  pamoja na Donata miaka (26).
Baadhi ya Mashuhuda wa ajali hiyo walieleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi ambapo dereva wa basi hilo alishindwa kulimudu na hatimae kugonga gari la kushindilia barabara na hatimae kupinduka.
Hadi tunakwenda mitamboni, Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza alikuwa hajapatikana ili kuthibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
BINAGA MEDIA BLOG.
Newer Post Older Post Home