BORESHENI HALI YA WAFANYAKAZI:AMNESTY.

By | 02:25
                     
Maandalizi ya kombe la Dunia
Shirika la kupigania haki za binadamu la Amnesty International ,linasema Qatar inalazimika kuboresha hali ya wafanyakazi wahamiaji wakati huu nchi hiyo inapoendelea na maandalizi ya kombe la dunia la mwaka 2022.

                    
Wafanyikazi wa kigeni ndio wanaotumika kujenga viwanja Qatar
Amnesty wanasema Qatar imepiga hatua kidogo sana kutekeleza ahadi nyingi walizozitoa mwaka jana, kwani wafanyakazi bado wanahitaji ruhusa kutoka kwa waajiri wao ,kubadili ajira au kuondoka nchini humo,mabadiliko ya malipo kwa wafanyakazi yanafanyika taratibu mno wakati ni jambo la muhimu mno.
                 
Newer Post Older Post Home