Tetemeko
kubwa la Ardhi limetikisa tena Nepal ,takriban majuma mawili tu tangu
tetemeko lingine kubwa zaidi kusababisa vifo vya zaidi ya watu 8000.
Watafiti wanasema kuwa kitovu cha tetemeko hilo lililikuwa katika mji wa Namche Bazar, karibu zaidi na mlima mrefu zaidi duniani Mlima Everest.
Kulingana na idara ya masuala ya ardhi na mazingira ya Marekani tetemeko hili lipya limefikisha kipimo cha 7.4.
Madhara ya tetemeko hili hayajabainika ila inasemekana kuwa lilitikisa mji mkuu wa India New Delhi, vilevile mji mkuu wa Bangladesh Dhaka.
Majumba yaliyosazwa na tetemeko la awali katika mji mkuu wa Nepala Kathmandu, yalitikiswa mno na tetemeko hili la hivi punde.
''Jamani mungu atuokoe maanake tetemeko hili la hivi punde lilikuwa lakutisha zaidi.
lilikuwa kubwa mno ''anasema Prakash Shilpakar mkaazi wa Kathmandu
Kitovu cha tetemeko hilo inadaiwa kuwa takriban kilomita 83km Mashariki mwa Kathmandu, eneo lililoko karibu na mpaka wa China.
