OWENS KUSIMAMIA FAINALI KOMBE LA DUNIA LA RAGA.

By | 04:18

Nigel Owens

Image copyrightGetty
Image captionNigel Owens anatoka Wales


Owens alisema kupitia mitandao ya kijamii kwamba anashukuru sana kutunukiwa hadhi hiyo.
New Zealand walicharaza Afrika Kusini 20-18 Jumamosi na watakutana na Australia, waliowashinda Argentina 29-15 Jumapili.
Mataifa hayo mawili hayajawahi kukutana kwenye fainali.
Mwingereza Ed Morrison, aliyekuwa refa fainali ya 1995 kati ya Afrika Kusini na New Zealand, na raia wa Ireland Alain Rolland, aliyesimamia fainali kati ya England na Afrika Kusini 2007, ndio marefa wengine kutoka kaskazini waliowahi kusimamia fainali ya dimba hilo.
Mwakilishi wa New Zealand jopo la kuteua refa wa kusimamia fainali Bw Grant Fox alikuwa tayari amedokeza kwamba Owens angesimamia mechi hiyo ya Oktoba 31 uwanjani Twickenham.
Newer Post Older Post Home