The Latest






By Julius Mathias, Mwananchi
Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza matokeo ya awali ya urais kwa majimbo matatu yaliyokamilisha mchakato huo mpaka jana asubuhi.
Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva aliyataja majimbo hayo kuwa ni Makunduchi, Paje na Lulindi.
Jaji huyo alisema, Makunduchi lilikuwa na wapigakura 12,742 waliojitokeza ni 10,682 sawa na asilimia 83.83 na hakuna kura zilizoharibika.
Jimboni humo; ACT-Wazalendo imepata 22, ADC 58, CCM 8,406, Chadema 1,769, Chaumma 68, NRA 23 na TLP na UPDP vimepata 18 kila kimoja.
Jimboni Paje kulikuwa na watu 10,276 na waliojitokeza ni 8,326. Kura halali ambazo wagombea husika waligawana zilikuwa 8,047.
ACT ilivuna kura 36, ADC 21, CCM 6,035, Chadema 1,899, Chaumma 28, NRA na TLP nane kila kimmoja na UPDP saba.
Huko Jimbo la Lulindi waliojiandikisha ni 59,027 na walijitokeza ni 45,844 ila kura 1,507 ambazo ni sawa na asilimia 3.29 ziliharibika.
Katika jimbo hilo ACT imepata 528, ADC 362, CCM 31,605, Chadema 11,543, Chaumma 179, NRA na TLP 43 kila kimoja huku UPDP kikivuna kura 34.


Scioli MacriImage copyrightAFP
Image captionDaniel Scioli (kushoto) na Mauricio Macri (kulia) watakabiliana kwenye duru ya pili
Wapiga kura nchini Argentina watashiriki duru ya pili ya uchaguzi mwezi ujao baada ya kukosekana kwa mshindi wa moja kwa moja katika duru ya kwanza Jumapili.
Mgombea anayeegemea siasa za mrengo wa kati-kushoto Daniel Scioli aliongoza kwenye kura za mapema, akimpiku mgombea anayeegemea siasa za kati-kulia na ambaye alikuwa meya wa Buenos Aires Mauricio Macri.
Wengi walitarajia Scioli aongoze kwa kura nyingi, lakini hilo halikuwa.
Duru ya pili ya uchaguzi itafanyika Novemba 22, na itakuwa mara ya kwanza kwa mshindi wa uchaguzi wa urais kupatikana kupitia duru ya pili nchini Argentina.
Baada ya kuhesabiwa kwa 86% ya kura, Scioli alikuwa mbele akiwa na asilimia 35.9%, Bw Macri naye akiwa na 35.2%.
Ili kushinda katika awamu ya kwanza, mgombea alihitaji kushinda 45% ya kura zilizopigwa, au apate angalau asilimia 40% na awe mbele ya mpinzani wa karibu kwa zaidi ya asilimia 10.
"Kilichofanyika leo kitabadilisha siasa za humu nchini," Bw Macri, meya wa Buenos Aires, ameambia wafuasi wake.
Bw Scioli aliteuliwa kugombea urais na rais anayeondoka Cristina Fernandez de Kirchner, ambaye haruhusiwi kuwania baada ya kuhudumu mihula miwili.

A woman leads donkeys with loads of firewood at
A woman leads donkeys with loads of firewood at Nessuit in Njoro, Nakuru County on October 7, 2015. The firewood sourced from the Nessuit Block of the Mau Forest. The Ogiek community living in this area will be trained on ways of adapting to climate change and using modern farming methods. PHOTO | SULEIMAN MBATIAH | NATION MEDIA GROUP 

By MORAA OBIRIA
The Ministry of Agriculture has embarked on sensitisation drives aimed at enlightening the Ogiek community on sustainable ways of adapting to climate change.
Phillip Owiti an apiculture officer with the ministry said the Ogieks need to be empowered with knowledge and skills in modern farming in order to survive in the changing environment.
“Climate change is everywhere and the Ogiek are not spared either.
“It is therefore important that they are enlightened to cope with it,” said Owiti in an interview with the Nation.
Change of biodiversity and rainfall patterns has not spared the traditional livelihoods of the Ogiek community inhabiting the environs of the Mau Forest complex.
The Ogieks mainly draw their livelihoods from bee keeping, producing volumes of honey to supplement their dietary needs from wild meat and fruits.
DESTRUCTION OF FOREST
However, the extensive destruction of the forest resulting to loss of the indigenous trees providing nectar for the bees and the drying of rivers that supported the trees has made their traditional methods of bee keeping impossible.
Mr Owiti said the traditional methods of bee keeping are no longer productive with the changing climate and habitat.
“Traditional bees are no longer as productive as they were before due to the unsuitable habitat,” he said.
He said they could expand their knowledge on bee keeping and enable them diversify into agri-business.
Mr Owiti said they will train them on adding value to honey, modern farming and marketing their produce, among other things.
The training will be regularly conducted with those living in Mariashoni and Nessuit wards being among the beneficiaries.
Further, Nakuru’s department of environment is planning to educate them on the use of eco-friendly sources of energy in order to reduce the rate of deforestation within the forest complex.
County Director for Environment Timothy Kiogora said conserving the Mau Forest complex would be impossible without the involvement of the local communities


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema hajahama Chama Cha Mapinduzi (CCM) kama ambavyo imekuwa ikidaiwa na baadhi ya watu na mitandao ya kijamii kwamba amejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
 
Pinda alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti juzi na wakazi wa Majimbo ya Mpanda Mjini na Kavuu kwenye mikutano minne ya hadhara iliyofanyika katika kata za Kakese, Kibaoni, Usevya na Majimoto wakati akifunga kampeni za uchaguzi mkoani Katavi.
 
“Kuna picha zimesambaa mitandaoni zinadai nimehamia Chadema. Hivi kweli sasa hivi nahamia huko ili iwe nini?” Alihoji.
 
Alisema picha wanazozisambaza ni za mwaka 2012 ambazo zilipigwa wakati akionyesha kwa wananchi moja ya kadi alizopokea kutoka kwa wanachama wa Chadema. Katika moja ya picha hizo, Waziri Mkuu Pinda anaonekana akiwa na mlinzi wake huku akionyesha kadi ya Chadema.
 
Hata hivyo, hakuna kiongozi yeyote wa Chadema anayeonekana akimkabidhi kadi kama mwanachama mpya.
 
CHANZO: NIPASHE



Kocha wa Man United, Louis Van Gaal akipeana
Kocha wa Man United, Louis Van Gaal akipeana mkono na kocha wa Man City mara baada ya kipenga cha mwisho cha mwamuzi aliyechezesha mechi ya mahasimu hao wa jijini Manchester iliyokwisha kwa matokeo ya 0-0. 

Manchester, England. Timu hasimu za jiji la Manchester, United na Manchester City zimeshindwa kutambiana baada ya kulazimishana sare ya 0-0  katika mchezo wa jana wa Ligi Kuu England.
Man United  ilikuwa na mchezo mzuri na kuutawala kwa kiasi kikubwa mchezo huo, lakini  ilishindwa kutumia faida hiyo ya kucheza nyumbani kuifunga Man City  iliyonekana kumkosa mshambuliaji wao hatari, Sergio Aguero aliye majeruhi.
Kwa matokeo hayo,  Man City imerudi kileleni mwa  Ligi Kuu  Englandkwa tofauti ya mabao dhidi ya Arsenal iliyoongoza kwa muda baada ya ushindi wao wa juzi wa mabao 2-1 dhidi ya Everton.
Katika michezo mingine iliyochezwa jana, Tottenham  au Spurs iliinyuka Bournemouth kwa mabao 5-1, wakati Sunderland  ikiibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Newcastle.
Mechi nyingine ilikuwa baina ya Liverpool na Southampton zilizokuwa zikicheza jana usiku.




Wapiga kura wakihakiki majina yao
Wapiga kura wakihakiki majina yao 

By Joyce Mmasi, Mwananchi
Dar es Salaam. Shughuli za upigaji kura katika kituo cha EDP kilichoko eneo la Kimara Stop Over jana zilisimama kwa muda na wapigakura kufungiwa ndani ya kituo baada ya kukosekana kwa karatasi za kupigia kura za mgombea urais.
Msimamizi msaidizi wa kituo hicho, Jastina Khatibu alikiri kuwapo kwa changamoto hiyo akisema badala yake, wapigakura hao walitakiwa kupiga kura ya ubunge na udiwani.
Alisema wapigakura hao, walilazimika kusubiri kwa muda ili kupiga kura ya urais.
Kituo cha EDP kina vituo vidogo vinane vyenye wastani wa wapiga kura 450.
Hadi jana saa 4:00 asubuhi kilikuwa bado hakijafunguliwa kuanza kazi.
Msimamizi mkuu wa kituo hicho Julias Nyamhonga alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iliwasilisha vifaa pungufu tofauti na matarajio yao.
Katika kituo cha Temboni, wananchi zaidi ya 400 wenye majina yanayoanzia na herufi P walikwama kupiga kura kwa madai kile walichosema majina yao yapo kituo kingine umbali wa zaidi ya kilometa mbili.
Hata hivyo kulitokea sintofahamu baada ya majina ya wananchi hao kukosekana kwa mara nyingine katika kituo walichokwenda kuyaangalia.
Hata hivyo, hawakupatiwa msaada na kukosa haki ya kupiga kura licha ya kuwa na vitambulisho.
Msimamizi wa Kituo cha Temboni, Albert Feni alisema kati ya vituo 18 vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya upigaji kura ni vituo 10 pekee vilivyokuwapo.
Katika Kituo cha Shule ya Msingi Saranga wananchi walianza kupigia kura saa 8.12 mchana kutokana na kushindwa kuwatambua wapigakura baada ya kukosa daftari lenye orodha ya majina yote.
Msimamizi wa kituo hicho, Rukia Aziz alisema daftari hilo lilipotea hivyo kuwalazimu kwenda kufuata lingine (NEC).






Jamii zetu za Kiafrika zilikuwa na taratibu nzuri za kumwadhibu mtoto kwa lengo la kumfundisha pindi anapokosea. Taratibu hizi zililenga kumpa mtoto uzoefu kwa kumjenga kukabiliana na changamoto za maisha yaliyomzunguka.
Viboko na nguvu wanayotumia wazazi wa leo haikuwa kati ya njia walizotumia wazee wetu katika kujenga tabia za watoto wao. Wazazi/walezi wa leo hutumia njia ya fimbo au kipigo cha aina yoyote ili kumkanya au kumkomesha mtoto asirudie tena. Leo tutaangalia madhara ya kumpiga mtoto ili awe na adabu na kama zipo namna tunaweza kutimiza majukumu yetu ya kuhakikisha mtoto anakuwa na tabia njema bila kutumia nguvu.
Mtaalamu na mwandishi mahiri katika saikolojia ya makuzi ya mtoto Sarah Kovac anasisitiza kuwa kumpiga mtoto mfano kwa fimbo, vibao, ngumi, mateke na kadhalika kwa malengo ya kumfundisha mtoto asirudie kosa humuumiza mtoto kimwili, kisaikolojia, na mara nyingi humfanya mtoto kutokujiamini na hata kupunguza ukaribu na mlezi/mzazi bila kupata mafunzo yoyote au kuelewa chochote kwenye kosa husika.
Uzoefu unaonyesha kwamba kumuumiza mtoto kwa lengo la kumkomesha hakumjengi kujirekebisha kitabia bali mara nyingi humfanya kuigiza tabia njema kwa muda tu na kuficha makucha ya tabia mbaya.
Vilevile humfanya mtoto asiweze kujisimamia mwenyewe kutenda mema mpaka atishiwe adhabu ama kipigo. Yaani ukitaka kumtuma mwanao kijiko kwa mfano, lazima useme, ‘usipoleta kijiko nitakuchapa.’
Wataalamu wa makuzi wanakubaliana na taratibu tulizozitupa za mababu zetu zilizolenga kutoa adhabu stahiki ili kumfunza mtoto aweze kudhibiti tabia yake, kung’amua kati ya jema na baya mwenyewe na kufanya jambo si kwa kuogopa adhabu bali kwa kujua kuwa ni jambo sahihi kufanya. “Unavyoongeza kuwapiga watoto (kila wanapokosea), wanazidi kupoteza uwezo wa kujisimamia wenyewe. Mara nyingi wanazoea kusimamiwa na wazazi, walezi n.k. lakini je, kama hamna anaewaangalia na kuwasimamia, utegemee nini?” Anauliza Sarah Kovac.
Aina ya adhabu unayoitumia kumkanya mtoto siku zote imjengee uwezo wa kuwa na nidhamu popote pale alipo, uwepo -usiwepo. Ifike mahala mtoto asidanganye siyo kwa kuwa atachapwa akidanganya ila kwa kuwa anaelewa kusema uongo siyo jambo jema.
Tumia fursa hii kujenga uwezo wa mtoto kutatua matatizo yake na ya watu wanaomzunguka. Fursa ya aina hii inaondoa uwepo wa nidhamu ya uoga na atafanya mambo bila kuwa na wasiwasi wa kupigwa, kufokewa au kudhalilishwa kwa namna yoyote. Watoto wa aina hii huwa na uwezo mkubwa wa kudadisi na kujifunza mambo mapya kwa uhakika wa kurekebishwa kwa upendo na kuonyeshwa njia sahihi ya kufanya mambo pale anapokosea. Malezi ya namna hii humpa mtoto moyo wa uthubutu katika maisha.
Mfano, ikitokea ameharibu labda kifaa cha umeme, usighadhibike kupita kiasi bali tumia fursa hii kumuelewesha asiharibu tena. Muelezee namna ya kutumia kifaa hicho kwa ufasaha, manufaa yake na gharama za kununua kingine au kukitengeneza. Hii itumike kwa mtoto anayeelewa (mkubwa kiumri kuanzia miaka mitatu na kuendelea).
Kwa mtoto asiyeelewa (mdogo), weka vifaa kama hivi mbali naye. Njia hii humfanya mtoto kutokuviogopa vifaa hivi na kuvizoea na humuongezea udadisi. Huwezijua, pengine siku moja mtoto wako atakuja kuwa mhandisi mzuri wa kutegemewa na taifa kwa kuwa haukuua udadisi wake akiwa mdogo.
Makala haya yameandaliwa na wataalamu wa makuzi toka C-Sema .
MWANANCHI.


Image copyrightAFP
Image captionKibarua cha Tim Sherwood chaota nyasi
Klabu ya soka ya Aston Villa imemfukuza kazi Meneja wake Tim Sherwood baada ya kushika wadhifa huo kwa Miezi minane.
Sherwood alishuhudia timu yake ikiendelea kupoteza mchezo katika ligi kuu ya England kwa kuchapwa na Swansea kwa mabao 2-1.
Kocha wa timu ya vijana chini ya Miaka 21 wa Aston Villa, Kevin MacDonald, ndiye atakayeshika Umeneja kwa muda mpaka kupatikana kwa kocha mpya
Meneja wa zamani wa Everton na Manchester United David Moyes, ametajwa katika orodha ya makocha wanaohitajika kuchukua nafasi hiyo.
Sherwood aliteuliwa kuwa Meneja Mwezi Februari Mwaka huu kumbadili Paul Lambert na kufanikiwa kuwapeleka Villa Fainali ya FA CUP na pia kuwanusuru kushushwa Daraja toka Ligi Kuu England walipomaliza Nafasi ya 17.

Image captionAustralia yaichapa Argentina mchezo wa Raga
Timu ya taifa ya Australia ya mchezo wa raga imetinga hatua ya fainali ya michuano ya kombe la dunia la mchezo huu.
Australia walishuka dimbani kukabiliana na timu ya taifa ya Argentina na kuibuka kidedea kwa pointi 29 dhidi ya 15 za wapinzania wao.
Mchezaji mahiri wa Australia Adam Ashley-Cooper, aliisaidia timu yake kupata alama 13 za kuongoza mchezo huu wa nusu fainali.
Australia itapamba na New Zealand katika mchezo wa fainali utakaofanyika Octoba 31 huku michezo ya mshindi wa tatu ikifanyika Octoba 30.


Maldives
Image copyrightReuters
Image captionMke wa Rais Yameen alijeruhiwa kwenye mlipuko uliotokea Septemba 28
Makamu wa rais wa Maldives amekamatwa kuhusiana na jaribio la kumuua rais wa taifa hilo, waziri wa masuala ya ndani nchini humo amesema.
Ahmed Adeeb anazuiliwa na karibuni atashtakiwa kwa uhaini, Umar Naseer amesema kupitia Twitter
Rais Abdulla Yameen alinusurika kifo baada ya boti aliyokuwa akitumia kusafiri hadi mji mkuu akitoka kuhiji Mecca mwezi jana kulipuliwa.
Misukosuko ya kisiasa imekuwa ikiyumbisha Maldives miaka ya hivi majuzi.
Mzozo ulizuka baada ya Yameen kushinda uchaguzi, wapinzani wakisema kulikuwa na udanganyifu.
AdeebImage copyrightAFP
Image captionAdeeb amekamatwa baada ya kuwasili uwanja wa ndege
Maafisa wakuu wa polisi walifutwa kazi kutokana na uchunguzi wa mlipuko huo, wiki moja baada ya rais huyo kumfuta kazi waziri wake wa ulinzi.
Polisi wamethibitisha kwamba walimkamata Bw Adeeb akiwa uwanja wa ndege baada yake kurejea kutoka safari ng’ambo.
Bw Yameen hakuumia kwenye shambulio hilo la Septemba 28, lakini mkewe, msaidizi mmoja na mlinzi walijeruhiwa.