Dar es Salaam. Baadhi ya
wananchi wamekuwa na maoni tofauti kuhusu namna sakata la
wizi wa fedha kwenye akaunti ya Escrow linavyoshughulikiwa, huku wengine wakisema
umefika wakati sasa nchi iongozwe na rais dikteta.
wizi wa fedha kwenye akaunti ya Escrow linavyoshughulikiwa, huku wengine wakisema
umefika wakati sasa nchi iongozwe na rais dikteta.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, walisema
kuwa uamuzi wa Naibu Spika,
Job Ndugai kuwaomba wabunge kukishauri kiti chake juu ya hatua ya kuwasilishwa na
kujadiliwa kwa ripoti ya uchunguzi wa fedha za Escrow, umeonyesha Bunge linataka ukweli ujulikane.
Job Ndugai kuwaomba wabunge kukishauri kiti chake juu ya hatua ya kuwasilishwa na
kujadiliwa kwa ripoti ya uchunguzi wa fedha za Escrow, umeonyesha Bunge linataka ukweli ujulikane.
Mratibu wa Umoja wa Wanawake Wanasiasa Tanzania
(ULINGO), Dk Ave Maria Semakafu
alisema baadhi ya watu wanataka kupotosha ukweli kwa kuwataja viongozi wasiohusika hawahusiki
moja kwa moja na ufisadi wa fedha hizo badala ya kuwanyooshea kidole majaji waliotajwa kupewa
mgawo huo.
alisema baadhi ya watu wanataka kupotosha ukweli kwa kuwataja viongozi wasiohusika hawahusiki
moja kwa moja na ufisadi wa fedha hizo badala ya kuwanyooshea kidole majaji waliotajwa kupewa
mgawo huo.
Akizungumzia suala la mahakama kuzuia jambo hilo
kujadiliwa bungeni, alisema kinachofanyika ni
sawa na kumpa nyani kesi ya ngedere huku ukijua kabisa haki haitotendeka.
sawa na kumpa nyani kesi ya ngedere huku ukijua kabisa haki haitotendeka.
“Hata waandishi wa habari wanakosea mahali pa
kulenga, majaji watatu ndio wametajwa kupata
mgawo (anawataja), suala hapa Jaji Kiongozi atoe taarifa kuhusiana na jambo hilo,” alisema Semakafu.
mgawo (anawataja), suala hapa Jaji Kiongozi atoe taarifa kuhusiana na jambo hilo,” alisema Semakafu.
Alisema kutokana na kujirudiarudia kwa matukio ya
ufisadi nchini, taifa limepoteza mwelekeo hivyo
linahitaji kiongozi dikteta atakayeweza kuwashughulikia wahalifu bila huruma.
linahitaji kiongozi dikteta atakayeweza kuwashughulikia wahalifu bila huruma.
“Nchi haijulikani inakwenda au inarudi. Dawa ni
kupata kiongozi dikteta, nchi hii haihitaji mtu mwenye
makundi, tumefika hapa kwa sababu ya urafiki,” alisema Semakafu.
makundi, tumefika hapa kwa sababu ya urafiki,” alisema Semakafu.
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe,
Profesa George Shumbusho alisema
kinachoonekana sasa ni matokeo ya viongozi kutokuwa na utamaduni wa kuchukua hatua
kali watu wanapofanya makosa, ikiwamo kufilisi mali zao.
kinachoonekana sasa ni matokeo ya viongozi kutokuwa na utamaduni wa kuchukua hatua
kali watu wanapofanya makosa, ikiwamo kufilisi mali zao.
Profesa huyo alisema kwa hali ilipofikia nchi
inahitaji kupata kiongozi dikteta ambaye atakuwa
tayari kutawala kwa muda mfupi ili arudishe nidhamu iliyopotea.
tayari kutawala kwa muda mfupi ili arudishe nidhamu iliyopotea.
“Tunahitaji dikteta atakayesema nitakaa kwa muda
mfupi, asafishe uozo, kisha aondoke…
, Haiwezekani tuendelee kushuhudia nchi ikizidi kufilisika,” alisema Profesa Shumbusho.
, Haiwezekani tuendelee kushuhudia nchi ikizidi kufilisika,” alisema Profesa Shumbusho.
Mbunge wa Mgogoni, Kombo Khamis Kombo (CUF),
alisema matukio ya ufisadi
yameongezeka nchini kwa sababu kila kiongozi anayetarajiwa kuchukua hatua analalamika
kuwa watendaji wake wanamwangusha.
yameongezeka nchini kwa sababu kila kiongozi anayetarajiwa kuchukua hatua analalamika
kuwa watendaji wake wanamwangusha.
“Viongozi wanapiga danadana, wana watu ambao
hawawezi kuwakosoa…, tulipofikia tunahitaji
kiongozi mwenye maadili,” alisema Kombo.
kiongozi mwenye maadili,” alisema Kombo.
Mkuu wa Kitivo Msaidizi (Taaluma), Kitivo cha Sanaa na Sayansi
ya Jamii, Chuo Kikuu cha
Tumaini Dar es Salaam, Danford Kitwana alisema kilichotokea bungeni juzi kinaashiria Serikali
kujaribu kulizima suala la Escrow ili lisijadiliwe kwa kuwa wanafahamu linaweza kuwang’oa baadhi
ya viongozi madarakani.
Tumaini Dar es Salaam, Danford Kitwana alisema kilichotokea bungeni juzi kinaashiria Serikali
kujaribu kulizima suala la Escrow ili lisijadiliwe kwa kuwa wanafahamu linaweza kuwang’oa baadhi
ya viongozi madarakani.
Hata hivyo, alisema kutokana na kauli za wabunge
wengi waliotoa mapendekezo yao kutaka jambo
hili lijadiliwe na ukweli kufahamika, Serikali itakuwa na nafasi ndogo ya kukwepa kutekelezwa kwa
maoni ya wabunge walio wengi.
hili lijadiliwe na ukweli kufahamika, Serikali itakuwa na nafasi ndogo ya kukwepa kutekelezwa kwa
maoni ya wabunge walio wengi.
Aliongeza: “Tatizo la Tanzania ni ukosefu wa
maadili na uchungu wa mali ya umma, tutaendelea tu
kusikia kesi kama hizi kwani bado kuna mambo mengi yaliyofanywa bado hayajafichuliwa.”
kusikia kesi kama hizi kwani bado kuna mambo mengi yaliyofanywa bado hayajafichuliwa.”