
Rais wa Gambia yahya Jammeh aliyeepuka jaribio la mapinduzi.baadhi ya watu waliohusika na mapinduzi hao wameanza kukamatwa
Waliokamatwa ni pamoja na maafisa kadhaa wa kijeshi pamoja na raia.
Wanajeshi watiifu kwa rais, wanasemekana wamekuwa wakisaka nyumba za wapinzani wake.
Awali akiwa katika mji mkuu Banjul, Rais Jammeh alilaani washukiwa hao wa mapinduzi wanaosemekana kuungwa mkono na baadhi ya mataifa ya kigeni.