
Klabu za ligi kuu ya England zipo katika
maandalizi ya msimu ujao wa ligi kuu huku baadhi ya klabu zikianza
mchakato wa kusajili wachezaji wapya kwa ajili ya kutumikia klabu zao.
Di Maria bado ana mkataba na klabu yake
ya Manchester na huenda klabu hiyo ikamtoa kwa mkopo kwenda kucheza
kwenye klabu yoyote inayomtaka.
Bayern imesema ipo tayari kutoa ofa
kubwa zaidi ya iliyotangazwa na Paris St Germain ambayo nayo imepania
kumnyakua winga guyo raia wa Argentina.