Watafiti hao hata hivyo wanasema ni vigumu kufikia sasa kubaini iwapo athari hiyo ni sawa sawa miongoni mwa wanadamu.
Watafiti hao hata hivyo wanasema ni vigumu kufikia sasa kubaini iwapo athari hiyo ni sawa sawa miongoni mwa wanadamu.
Hilo linatokana na sheria kali zinazozuia utafiti wa aina hiyo.
Licha ya utafiti huu msemaji wa chuo cha afya ya watoto nchini Uingereza Dr Martin Ward-Platt, anaonya kuwa wanadamu hawapaswi kukatazwa kabisa kumeza dawa zilizo na Paracetamol kwa sababu zinasaidia sana kutibu mafua ya mara kwa mara na wakati mwengi kipimo kimoja au viwili vya Paracetamol vinatosha kutibu homa.
Daktari Sadaf Ghaem-Maghami, kwa upande wake ameonya kuwa utafiti huo haupaswi kukubalika pasi na maswali muhimu kuulizwa kuhusu ukweli wake.
''Licha ya kuwa matokeo ya utafiti huu ni mzuri na unavutia ,tunapaswa kufanya utafiti zaidi kwa sababu utafiti huu ulifanyiwa wanyama, Je mwili wa binadamu utaitikia vipimo vya dawa hii kwa njia sawa na hiyo ? alihoji dakta Sadaf.
Utafiti huo umechapishwa katika jarida la kisayansi na utabibu '' Translational Medicine''.