
Marta amefikisha idadi hiyo ya mabao baada ya kufunga bao moja kwa mkwaju wa penati kwenye mchezo wa timu yake dhidi ya korea kusini ambapo Brazili waliibuka kidedea kwa mabao 2-0.
Ushindi huo umeifanya Brazil kuwa vinara wa kundi E, Baada ya Hispania na Costa Rica kwenda sare ya kufungana 1-1.
Mshambuliaji huyu ameichezea timu ya taifa jumla ya michezo 137 akiwa kafunga mabao 93. Kwa sasa Marta ni mchezaji wa klabu ya Rosengard FC ya Sweden.