MAAJABU YA ULIMWENGU:PALE AMBAPO MCHUNGAJI ANAMUWA KUTOZA KIINGILIO KWA WAUMINI WAKE.

By | 05:14
Ni jambo la kushangaza na ni vigumu kukuta viongozi wa kanisa wakiwatoza waumini wao ada ili waweze kuhudhuria huduma ya neno la Mungu.
Lakini hii imetokea kwa waumini wa kanisa la Christ Embassy ambao wameonekana kutokua na furaha baada ya kutakiwa kulipa 1000 Naira ambayo ni fedha ya Nigeria kama kiingilio katika mkesha wa mwaka mpya ulioandaliwa na Mchungaji Chris Oyakhilome.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na PM News ilisema kwa wale ambao hawakua na uwezo wa kulipa kiasi hicho cha fedha walikua wakirudi majumbani ama kwenda sehemu nyingine kupata huduma ya neno la Mungu.
Chanzo hicho kilisema  sera hiyo ya kulipa kiingilio ndani ya kanisa hilo siyo mpya na ilishawahi kufanyika kwa mara nyingine mwaka mpya 2010 ingawa wengi hawakupendezwa na tukio hilo.
                      church
Hii imeonekana kama ubaguzi kwa wasio nacho na uongozi wa kanisa ulisema umeamua kufanya hivyo ili kupunguza wingi wa watu wakati wa mkesha wa kuupokea mwaka mpya.
“Kanisa lina uwezo wa kubeba waumini 20,000 na limeweza kutengeneza zaidi ya Naira milioni 20 kutokana na mauzo ya tiketi za kuingia kanisani kupata huduma hiyo”kiliongeza chanzo hicho cha habari.
Newer Post Older Post Home