TAZAMA PICHA MBALIMBALI ZA MKUTANO WA MH.LOWASSA JIJJINI ARUSHA.

By | 11:27
Na Kiyyian Ole Kiyiapi,

 Mgombea kiti cha Urais kupitia Chama cha demokrasia na maendeleo(Chadema) ,chini ya mwamvuli wa vyama vinavyounda UKAWA,CHADEMA,NLD,CUF,NCCR MAGEUZI,Mh.Edward Ngoyai Lowassa leo mchana aliweza kuhutubia mkutano wa hadhara katika ,viwanja vya Leganga-Usa river wilayani Arumeru Mashariki Jijini Arusha.
Lowassa aliambata na aliyekuwa Waziri mkuu mstaafu katika serikali ya awamu ya tatu ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Fredrick Sumaye,pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA),akiwemo muasisi wa Chama hicho mzee Edwin Mtei.

Mgombea ubunge kupitia chama hicho wilayani Arumeru Mashariki, Mh Joshua Nassari,na wagombea mbalimbali katika  nafasi ya udiwani walinadi sera zao,pamoja na kuomba kura,
Mh Edward Lowassa alinadi sera zake   akizitaja Elimu kuwa kipaumbele kwanza  ,elimu kuwa bure kuanzia chekechea hadi chuo kikuu,akiamini wananchi hawawezi kujikomboa kifikra kama hawajawezeshwa kielimu ili kuondoa ujinga na kuleta,maendeleo,kilimo kukiboresha,sekta ya afya kuboreshwa  katika ngazi zote za wilaya,kutatua kero ya migogoro ya ardhi,maji,umeme.
Baada ya mkutano huo ambao ulihudhuriwa na maelefu ya wakazi wa Usa river Mh.Edward Ngoyai Lowassa aliweza kuelekea katika viwanja vya sinoni kwa mkutano mwingine wa hadhara.
















picha zote na Kiyyian Ole Kiyiapi.
Newer Post Older Post Home